Information on this topic also available for:
Kuandaa upatanisho - Preparing for conciliation
| More information in Swahili |
Kuwa tayari na wazi kuhusu matokeo unayotaka ni njia nzuri sana kujitayarisha kupatanisha. Hii ni muhimu bila kujali kwa vyovyote kama wewe ni mwombaji au mshtakiwa.
Mashauri kumi juu ifuatayo yanaweza kukusaidia kuandaa na kupata faida zaidi kutoka njia ya upatanisho.
Mashauri kumi juu ya upatanisho
1. Fikiria kuhusu unachotaka
Fikiria kwa uangalifu kuhusu masuala yako na matokeo unayotaka kufaulu. Andika muhtasari ya masuala haya.
2. Panga jinsi unatakavyokubaliana
Uwe tayari kupokea mawazo na kubadilisha. Fikiria kuhusu masuala ya mtu mwingine na jinsi atakavyopokea maoni yako. Kupatana kunaweza kuhusisha kila upande kulegeza madai yake ili kufikia maafikiano ambayo yanafaa kwa nyote wawili.
3. Sema upande wako wa maelezo
Eleza kwa ufupi upande wako wa maelezo na onyesha ushahidi wako kwa mtu mwingine. Eleza jinsi unavyotaka kutatua mabishano. Lenga utatuzi. Jaribu kutobishana kuhusu nani ni sahihi au si sahihi, au maana.
4. Sikiliza mtu mwingine
Sikiliza kwa uangalifu mtu mwingine na angalia ushahidi wao. Labda utataka kuandika vidokezo. Umpe nafasi kuongea na usiingilie. Jaribu kufikiri maoni yao, hata usipoyakubali.
5. Lenga masuala, na sio hisia
Endelea kulenga masuala, na sio hisia au matendo ya mtu mwingine.
6. Anza kujadiliana
Anza kuwaza utatuzi unaowezakana. Fanya fadhila na fadhila ya kujibu fadhila. Upatanisho wa mafanikio unatokea wakati upande wote wawili wanapokubali utatuzi.
7. Kubali tu kwa mambo unayoona yanafaa
Uwe na hakika unakubali kwa matokeo pekee unayoona yanafaa. Kumbuka kwamba lazima kuwa na maafikiano katika kufika mapatano.
8. Omba kwa msaada kama una matatizo
Kama una matatizo, omba Mwamuzi, Mjumbe wa Baraza au Afisa wa Usajili kwa msaada. Kama ukijisikia kutishwa na mtu mwingine yule, umwambie Mwamuzi au afisa wa ulinzi mara moja.
9. Ukifika mapatano
Andika mapatano yako kwa fomu inayotolewa. Kama Mwamuzi amepatikana anaweza kukusaidia kuyaandika. Kabla mapatano yako kuwa amri ya kisheria ya lazima kufuatwa, utaulizwa kama unaelewa mapatano, na kuhakikisha umekubali kwa hiari.
10. Usipofika mapatano
Usipofika mapatano, hukumu itaendelea siku ile au tarehe ya baadaye. Fikiria kama masuala yako ni muhimu ya kutosha kurudi siku nyingine inavyoweza kuzidisha muda, gharama na usumbufu kwako.
Get a free copy of Adobe Acrobat Reader so you can access PDF versions of our information.